Monday, May 26, 2014

Soko Kuu la Kariakoo na umri wake wa miaka 40

 Soko Kuu la Kariakoo ambalo linasimamiwa na Shirika la Masoko ya Kariakoo (SMK) tangu mwaka 1974; kwa mujibu wa Sheria Na.36 ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.Shirika hili itakapofika tarehe 8/12/1914 litakuwa linatimiza miaka 40 tangu Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius K.Nyerere alipofungua rasmi shughuli za uendeshaji wa Shirika hili hapo tarehe 8/12/1974.
Kila mahali huwa na taratibu zake za kiutendaji katika kusimamia watu,katika picha hapo juu utaona baadhi ya askari wa Shirika wakiwa katika ukaguzi wa mpangilio wa bidhaa ambazo wafanyabiashara hupanga katika maeneo yao tofauti na taratibu za Shirika.Wafanyabiashara hawa wakati mwingine baadhi yao huvuka alama za mistari ambayo imechora kuwaonesha mipaka ya  sehemu zao; hivyo hulazimika maaskari hawa kufanya operesheni ya kukagua maeneo mbalimbali ili kuwarekebisha wale wanaokuwa wamekiuka utaratibu huo wa upangaji bidhaa zao.

No comments:

Post a Comment