Tuesday, April 8, 2014

Kutoka Kariakoo leo Jioni

 Katika picha hizi utaona ni Timu ya Menejimenti pamoja na Wafanyabiashara wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Shirika la Masoko ya Kariakoo,hapa walikuwa wakipewa mrejesho wa kikao ambacho kilikuwa kimefanyika Kwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ofisini kwake na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala. Hii imekuja baada ya uharibifu ulifanyika katika Soko la Kariakoo mwishoni mwa wiki iliyopita.
 Wajumbe wa Menejimenti ya Shirika la Masoko ya Kariakoo pamoja na Ujumbe wa Wafanayabiashara kwa pamoja wakiwa wanasikiliza mrejesho wa Kikao baina ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala,Mkuu wa Wilaya ya Ilala na Ujumbe wa Shirika la Masoko ya Kariakoo ulioongozwa na Meneja Mkuu wa   Shirika la Masoko ya Kariakoo. Katika kikao hiki Meneja Mkuu hakuwepo badala yake aliwakilishwa na Meneja wa Fedha ambaye aliambatana naye.
Mfanyabiashara Mzee Mwinyishehe mwenye kofia akiwa anamsikiliza mjumbe mmojawapo alipokuwa anachangia mawazo na kuishukuru timu nzima iliyokuwa imeambatana na Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo. Mrejesho wa kikao hicho uliwasilishwa na Mrs.Marieta Masaua Meneja wa Fedha kwa niaba ya Meneja Mkuu wakisaidiana na Mzee Mwinyishehe kama Muwakilishi wa Wafanayabiashara na  Kaimu Mhandisi wa Shirika Bwana Flavian Mlelwa