Tuesday, June 16, 2015

Miradi ya Wanamtandao wa 2SEEDS Network

 Katika picha hapo juu ni Wanamtandao wa 2SEEDS Network,akina mama hawa wamekuwa wakijituma kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha wanafikia malengo yao ya Kikundi. Wanamtandao hawa wapo katika Kijiji cha Tabora nje kidogo ya Wilaya ya Korogwe.Wanamtandao wanajishughulisha na utengenezaji wa Crips za viazi,karanga zenye mchanganyiko na mayai na wanakausha mboga za majani kwa kutumia mashine za bei nafuu, amabayo kila mwanamtandao katika kikundi anamiliki.
Mradi katika picha hapo juu unavyojaribu kuelezea malengo ya miradi yote ni kuwabadilisha maisha yao Wanamtandao.
Kijungumoto mradi pekee miongoni mwa miradi nane, wenye kutoa asali na nta na umekuwa wenye mafanikio makubwa sasa tangu umeanzishwa na tayari Wanamtandao wameanza kufaidi matunda yake.