Thursday, February 12, 2015

Hawa madogo vipi unawafahamuuuuuuuuuuu?

 Hawa watoto ambao wana rika yakuwa shuleni wanasoma!Lakini huonekana wakizurula ndani ya Soko Kuu la Kariakoo! Jambo ambalo huwapa wakati mgumu hata wateja mbalimbali wanaofika hapa sokoni kujipatia mahitaji mabalimbali!



 Asilimia kubwa ya watoto hawa wakihojiwa wanakotoka hutoa majibu kuwa wanatokea mkoa wa Tanga, na jambo la kusikitisha utafiti mdogo uliofanyika watoto hawa hufika hapa Sokoni kwa usafiri wa malori na tena wakiwa na umri dogo kati ya miaka 11 hadi 13, hivyo basi hukulia katika mazingira haya ya hapa Sokoni wakijishughulisha na kazi za hapa na palee!kujikimu kimaisha!
Katika picha hizo zote hapo juu ni watoto kadhaa waliokamatwa na Maafisa Usalama wa Shirika la Masoko Kariakoo mapema leo asubuhi! Basi ndugu Watanzania anayehusika na mtoto mmojawapo kati ya hao waliopo katika picha hizo, karibu ufike sokoni hapa Kariakoo ili uweze kumpata!

Kinachoendelea -Kariakoo Market Corporation

 Bwana Paul Nsimbila Mkufunzi mwenye laptop akiwa katika Ukumbi wa Shirika la Masoko wakati akiendesha semina kwa watumishi wa Shirika kuhusu Sheria mpya ya manunuzi na kanuni zake.
 Watumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoowaliohudhuria mafunzo ya kuhusu Sheria mpya ya manunuzi wakiwa wanafanya swali mojawapo alilowapa Mkufunzi Bwana Paul Nsimbila jana asubuhi, kama sehemu ya mazoezi
Watumishi katika makundi ya watu wawiliwawili wakiendelea na zoezi la kujibu swali mojawapo alilolitoa kama sehemu ya mazoezi katika mafunzo.