Tuesday, August 26, 2014

Usafi katika Soko Kuu la Kariakoo-Dar Es Salaam

Katika picha hapo juu ni Mtumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Amiri Magala akiwa anaendelea na shughuli yake ya kusafisha moja ya mifereji ya maji taka iliyopo eneo la Shimoni. Uongozi wa Shirika huzingatia sanaa suala zima la Usafi katika maeneo yote ya Soko Kuu la Kariakoo ambalo ni maarufu sana kwa kupokea bidhaa mbalimbali za mazao kutoka mikoani.Kwa kuzingatia hilo mifereji hii ya maji taka  hukaguliwa mara kwa mara kila siku ili kuhakikisha maji taka yanatoka na kuingia katika mfumo mkuu wa Jiji wa maji taka.

LEEKS ni nini?

Kwa wale wataalam wa mapishi na vyakula hawataweza kushangaa sana kuwa majani haya ni ya nini?au majani gani?
Hii ni mojawapo yambogamboga za majani za kisasa zinazoitwa LEEKS hizi hupatikana pia hapa sokoni Kariakoo kwa wingi sanaa! Fika Sokoni Kariakoo eneo la Shimoni katika meza za mbogamboga! zikiwa bado fresh utazipata! Karibu sanaaaa!

ZUKIN na BLUKOLIN

Katika picha hapo juu sio matango; ila ni moja ya mboga aina ya ZUKIN na BLUKOLIN.Aina hzi za mbogamboga huzalishwa kwa wingi katika mikoa ifuatayo; Morogoro,Tanga  katika wilaya za  Lushoto,Korogwe  na  kule Arusha.Fika Sokoni Kariakoo eneo la Shimoni utazipata kwa wingi na bei yake ni nzuri. Karibuni sana!