Friday, April 4, 2014

Uharibifu umeendelea tena usiku wa kuamkia leo katika Shirika la Masoko ya Kariakoo

 Katika picha hapo juu ni sehemu ya Pampu ya maji ambayo ilikuwa inatumika kusukuma maji katika kisima ambacho kipo eneo la Soko dogo la Kariakoo.Pampu hii imevunjwa usiku wa kuamkia leo na Burudoza la Manispaa ya Ilala katika zoezi lao.Ndugu Msomaji Pampu hii ilikuwa ndani ya kiwanja cha Shirika la Masoko ya Kariakoo;lakini ndiyo hivyo imevunjwa.
 Katika picha hapo juu ni Watumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Flavian Mlelwa na Denis Mfuruki kutoka Kitengo cha Uhandisi wakifungua mabomba ya maji yaliyokuwa yameunganishwa na Pampu amabayo imevunjwa .Kuvunjwa kwa Pampu hii kumelitia hasara kubwa  Shirika  la Masoko.
Hapa katika picha Wahandisi wa Shirika wakimalizia kufungua nyaya za umeme ambazo zilikuwa zinatumika kupeleka  nishati ya umeme kwenye Pampu ya maji ambayo imevunjwa.