Friday, May 2, 2014

Kutoka Soko Kuu la Kariakoo! Teknolojia kuboresha upatikanaji wa Taarifa muhim

Katika picha hapo juu ni miongoni mwa Wafanyabiashara wa Sokoni Kariakoo eneo la Shimoni wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Shirika la Masoko Bwana Vedastus Valentine kulia mwenye miwani na  Romana Lukanga wa pili kutoka kulia. Hapa walikuwa wakigawa T-Shirts zinazohamasisha ukusanyaji bei halisi (KMC Database)
 Kwa muda mrefu imekuwa Wanafunzi wa vyuo na Watafiti mbalimbali wamekuwa wakipata  shida kwa kiasi fulani katika kupata takwimu sahihi za kuhusu mazo mbalimbali yanayozalishwa hapa nchini na kuingizwa katika masoko ya  hapa Jijini Dsm. Lakini sasa katika kipindi cha muda mfupi ujao hali hiyo itatoweka kwani taarifa za kila siku zitakuwa zinapatika kwenye Mtandao wa Shirika la Masoko ya Kariakoo.
Shirika la Masoko  ya kariakoo sasa lipo mbioni kukamilisha na kuanza kutumia Mfumo wake wa  kukusanya na kutoa Taarifa (KMC Database System).Katika picha hapo juu ni miongoni mwa Wafanyabiashara ambao amabao watakuwa wanasaidiana na Watumishi wa Shirika katika ukusanyaji taarifa za bei kwa kutumia simu zao.
 Katika picha ya kulia hapo juu pamoja na watu wengine lakini pia yupo Project Cordinator kutoka Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali ya 2SEEDS Network Monique Galvalo alikuwapo katika zoezi la ugawaji T-Shirts (Promo Materials) hapa Sokoni Kariakoo  ili kuhamasisha ukusanyaji wa taarifa sahihi za bei za mazao mbalimbali.
Kwa baadhi ya wafanyabiashara ambao wamekuwa tayari kushirikana na Idara ya Biashara kutoa taarifa halisi za bei kuhusu bidhaa wanazouza kila siku ili ziweze kuhifadhiwa katika  Mfumo wa Taarifa wa Shirika.