Wednesday, May 6, 2015

Kutoka Kariakoo Soko Kuu Jijini Dar Es Salaam

 Katika picha hapo juu ni sehemu ya Wajumbe wa kikao cha pamoja kati ya watumishi wa Shirika la Masoko Kariakoo wakibadilishana mawazo na Vijana wa kutoka Mtandao wa 2SEEDS Network ambao walifika sokoni hapo mwishoni mwa wiki iliyopita kutemebelea soko hilo wakiongozwa na Bi.Anna ambaye katika picha anaonekana akifafanua jambo fulani katika kikao hicho.
 Picha hii hapo juu inaonesha sehemu ya Vijana wa 2SEEDS Network pamoja na Mkuu wa Kitengo cha ICT wakwanza kushoto Bwana Anderson Shaka, wakiwa wanafuatilia kwa umakini maelezo ya Afisa Biashara wa Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Vedastus Valentine pichani hapo haonekani.
 Bwana Vedastus Valentine wa kwanza kulia akitoa ufafanuzi wa jambo katika kikao mwishoni mwa wiki iliyopita.Anayesikiliza kwa umakini karibu nae ni Bi.Ana LĂȘ Rocha ambaye ni Mkurugenzi wa 2SEEDS Network hapa nchini Tanzania.

Katika picha hapo juu ni  Ujumbe kutoka Wilayani Mburu katika mkoa wa Manyara ulioongozwa na Afisa Biashara wa wilaya hiyo Bwana Jeremiah Mtagwa mwenye shati la rangi ya bluu waliposimama kujitambulisha katika kikao kifupi kilichofanyika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Shirika la Masoko Kariakoo
 Picha ya pamoja ya wajumbe wa kikao,mara baada ya kumaliza kikao ndani ya ukumbi wa Shirika la Masoko Kariakoo.
Katika picha hizo hapo juu ni wajumbe waliohudhuria kikao cha kubadilishana mawazo jinsi ya kuendesha miradi mbalimbali.Katika picha hapo waliokaa kutoka kushoto wa kwanza ni Omary Mdakama  kutoka Kitengo cha ICT Shirika la Masoko Kariakoo,wapili ni Bwana Vedastus Valaentine, wa tatu ni Mkulima mkubwa wa vitunguu wilayani Mburu aliyeambatana na  Bwana Jeremiah Mtagwa ambaye ni  Afisa Biashara wa Wilaya ya Mburu mkoani Manyara ambao wote kwa pamoja walifika katika Soko la Kariakoo kuona na kujifunza mambo mbalimbali katika uendeshaji wa soko hili kubwa.