Saturday, January 28, 2017

Ujumbe kutoka TAMISEMI na Jiji la DSM wakutana na Menejimenti ya Shirika

 Picha ya pamoja miongoni mwa Wajumbe waliohudhuria kikao cha kujadili mstakabali wa Shirika la Masoko ya Kariakoo. Miongoni mwao ni Kaimu Mkurugenzi wa Serikali za Mitaa kutoka TAMISEMI Bi.Mirium Mmbaga aliyevaa vazi la Kitenge.
 Picha ya pamoja miongoni mwa wajumbe waliohudhuria kikao maalum kilichojadili juu ya mwenendo mzima wa kiutendaji wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, pamoja na Viongozi kadhaa kutoka TAMISEMI na Halmashauri ya Jiji la Dar Es Salaam, pia ilikuwepo Menejimenti ya Shirika hili iliyoongozwa na Meneja Mkuu wa Shirika Bwana Hetsoni Msalale Kipsi mwenye suti nyeusi.
Katika picha hapo juu ni miongoni mwa Wajumbe wa kikao maalumu ambacho kilifanyika katika Ukumbi wa Shirika la Masoko Kariakoo wiki iliyopita. Kutoka kushoto wa kwanza  ni Bwana Eustard  Ngatale Mkurugenzi Msaidizi katika masuala ya Sheria kutoka TAMISEMI,Bwana Denisi Mfuruki yeye ni Mjumbe wa Bodi ya Shirika la Masoko Kariakoo,watatu ni Bi.Miriam Mmbaga ambaye ni Mkurugenzi kutoka TAMISEMI katika Idara ya Serikali za Mitaa,anayefuata ni Bi.Sipora J.Liana Mkurugenzi wa Jiji la Dar Es Salaam,Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Bwana Msongela  Palela na wa mwisho ni Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Hetsoni Msalale Kipsi.Kikao hiki kilikuwa kinajadili mikakati mbalimbali ya namna gani ya kuliwezesha Shirika kufanya mabadiliko katika utendaji wake kuliko ulivyo hivi sasa, ambapo halionyeshi kufanya vizuri.