Thursday, August 14, 2014

Habari toka Soko Kuu la Kariakoo leo!

Mazao ya  mbogamboga na Viungo yanapatikana kwa wingi sana katika soko Kuu la Kariakoo.Kama uonavyo katika picha hiyo hapo juu  ni baadhi tuu ya mazao ambayo huingia Sokoni kila siku .
 Dagaa hawa maalum wanaopatikana katika Ziwa Nyasa lililopo Kusini Magharibi mwa Tanzania;wana ladha ya kipekee sana wanapatikana pia katika Soko hili kubwa la Kariakoo eneo la Shimoni sehemu ya Wafanyabiashara wa dagaa.Karibuni mjipatie bidhaa hii muhim kwa afya ya familia yako.
 Shughuli za biashara katika Soko Kuu la Kariakoo hapa Jijini Dar es Salaam huanza mapema sana alfajiri kila siku.Hapa katika picha utaona Wafanyabiashara wa matunda mbalimbali wakiwa eneo la Shimoni wakiendelea na shughuli zao  za kibiashara kama walivyokutwa mapema alfajiri majira ya saa 11.30.
Magunia ya vitunguu yakiwa yamepangwa katika eneo la Soko la Jumla Shimoni Kariakoo Jijini  Dar Es Salaam.Vitunguu hivi majira haya vinatoka katika mikoa tofautitofauti ikiwamo Morogoro,Mbeya,Iringa na Dodoma pia.