Monday, August 24, 2015

Matukio katika Picha

 Katika picha hapo juu kutoka kulia ni Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Florens Seiya, Mwenyekiti wa TUICO tawi Bwana Dennis Mfuruki aliyesimama na Bwana Henry Rwejuna ambaye ni Katibu wa TUICO tawi, kwa pamoja wakiwa wanaendesha mkutano wa wafanyakazi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo mwishoni mwa wiki iliyopita. Ni moja ya mikutano ya kawaida ambayo imekuwa inafanyika kwa nia ya kujenga na kuimarisha mahusiano baina wafanyakazi wa shirika na Mwajiri wao, wakilenga zaidi hali ya mwenendo mzima wa Shirika.
 katika picha hapo juu ni vitunguu maji ambavyo ni moja ya bidhaa zinazouzwa hapa katika soko  Kuu la Kariakoo jijini Dar Es Salaam.Vitunguu maji hivi hufikishwa sokoni Kariakoo vikiwa vinatoka mikoa mbalimbali ya Tanzania kama vile Mbeya,Arusha,Iringa na Singida.
Picha hiyo hapo juu inaonyesha sehemu tuu ya Watumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo wakiwa wametulia huku wakifuatilia maelezo ya Meneja Mkuu wa Shirika ,pichani hapo juu hayupo wakati wa mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Shirika mwishoni mwa wiki iliyopita.