Monday, September 15, 2014

Kutoka Soko Kuu la Kariakoo - DSM

 Kitu gani ambacho ukifika katika Soko Kuu la Kariakoo hutakipataaaa? La hasha kuanzia nafaka,matunda,mboga mboga za majani hadi viungo vya kila aina.Katika picha hapo juu utaona Vitunguu swaum,Tangawizi,Ndimu na vinginevyo vipo kwa wingi mezani vikiwa katika ubora sana.Karibu Soko kuu la Kariakoo ujipatie bidhaa za kila aina. Bei ya vitunguu swaum na tangawizi ni kati ya Sh.4000 hadi 4500 kwa kilo moja.

 Miongoni mwa Watumishi wa Shirika la masoko ya Kariakoo ni Bwana Idd Mrope ambaye anaonekana katika picha hapo juu.Hapa yupo katika maeneo ya Ofisi za Shirika zilizopo katika ghorofa ya kwanza katika jengo la Soko Kuu.
Soko Kuu la Kariakoo ni Soko kubwa kuliko hapa nchini Tanzani,hii picha inaonesha sehemu mojawapo ya soko hili ambapo hapa barabara inayoingia katika eneo la soko la Jumla maarufu kama Shimoni.Eneo hili linaloonekana katika picha ni Geti Namba. 5 ambapo bidhaa karibu zote ambazo huingia hapa Sokoni hupitia hapa.