Tuesday, December 9, 2014

Kuelekea Sikukuu za Christmas na Mwaka mpya!

 Njegere ni moja ya bidhaa adimu na yenye kupendwa sana na watu wengi kwa matumizi ya chakula. Njegere huingia katika Soko Kuu la Kariakoo kutoka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania kama vile Morogoro,Iringa,Njombe na kwingineko. Bidhaa hii kuelekea sikukuu za Christmas na Mwaka mpya bado inapatikana kwa wingi hapa Sokoni  hasa eneo la Shimoni.katika picha hapo juu Mfanyabiashara alikutwa na mpiga picha akiwa amekwisha kuzimenya njegere zake tayari kwa kuwauzia wateja mbalimbali.

Sokoni Kariakoo kuna kila aina ya vyakula.Katika picha hapo juu nafaka mbalimbali ambazo huuzwa katika soko Dogo.Mfanya biashara huyu ameweka wazi hata bei za vyakula kwa kuzingatia madaraja au ubora wake.Tunapoelekea katika Sikukuu za mwisho wa mwaka bei za vyakula hazijabadilika sana! Karibuni Sokoni kwa manunuzi ya bidhaa mbalimbali.