Thursday, May 14, 2015

Mkutano wa Baraza kuu la Wafanyakazi

 Hapo juu katika picha ni Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko kariakoo Bwana Florens Seiya akifungua Mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi hapo jana mapema asubuhi. Mkutano huo ulifanyika katika kumbi wa mikutano wa Shirika .

 Katika picha hapo juu kutoka kushoto ni Bi.Matha Mnzava kutoka TUICO Mkoa wa Ilala, wapili ni Bwana Ibrahim Masha ambaye ni Katibu wa Baraza  la Wafanyakazi katika Shirika la Masoko, wa mwisho ni Bi.Emy Rweyendera kutoka Baraza la Usuruhishi -CMA, wote kwa pamoja wakiendelea kuratibu shughuli za mkutano huo ndani ya Ukumbi wa Shirika la Masoko Kariakoo.

 Katika picha hapo juu ni Bi.Emy Rweyendera akitoa semina fupi kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa wajumbe wawakilishi wa wafanyakazi katika baraza kuu la wafanyakazi katika Shirika la Masoko Kariakoo.Bi.Rweyendera ni Mtumishi kutoka CMA alikuja kusimamia uchaguzi huo.

 Bi.Matha Mnzava akiwa amesimama kujitambulisha kwa wajumbe wa Baraza muda mfupi baada ya Mwenyekiti wa baraza hilo kulifungua rasmi.

 Bi.Emi Rweyendera kutoka CMA  ambaye amesimama akiwa anaendelea na zoezi la kugawa karatasi  kwa wajumbe za kupigia kura hiyo jana.

 Sehemu ya wajumbe wa Baraza wakingojea karatasi za kupigia kura muda mfupi kabla ya uchaguzi huo kufanyika,mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Shirika la Masoko Kariakoo jana asubuhi kuanzia saa tano.

Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Florens Seiya akitangaza matokeo ya uchaguzi wa Wajumbe wapya watakao wawakilsha Wafanyakazi katika vikao vya Baraza kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia sasa. Uchaguzi huo ulisimamiwa na Bi.Emy Rweyendela kutoka Baraza la Usuruhishi (CMA) na Bi.Martha Mnzava kutoka TUICO Mkoa.