Tuesday, May 27, 2014

Karibuni Kariakoo Soko Kuu-Jijini Dar-Es Salaam

 katika picha hapo juu ni Katibu Muhtasi  katika Ofisi ya Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo Mrs.Grace Kahatano,kama alivyokutwa Ofisini kwake akiendelea na shughuli zake.
 Shirika la Masoko la Kariakoo lina Idara nyingi mabalimbali, katika Picha hapo juu ni Afisa Biashara Bwana Vedastus Valentine aliyekaa na Mtakwimu wa Shirika la Masoko Bwana Henry  Rwejuna wakiwa ofisini wakijadiliana jambo; wote hawa kwa pamoja wapo katika Idara ya Biashara.
Soko Kuu Kariakoo siyo tuu huuza vyakula pekee bali  ndani ya Soko hili kuna maduka mengi sana yanayouza Pembejeo za Kilimo zikiwemo mbolea,madawa ya kuulia wadudu pamoja na mitambo/machine mbalimbali zinazotumika kufanya kazi za Kilimo.katika picha hapo juu muuzaji mojawapo akiwa anaunganisha aina mojawapo ya kupulizia dawa shambani ili aweze kuifanyia majaribio kabla yakumuuzia Mteja wake. Kumbe Kariakoo ni Soko muhimu sanaa kwa kila mmojawetu ikiwa wewe ni Mlaji au Mzalishaji. Karibu sanaa Kariakoo Soko Kuu upate mahitaji yako.

No comments:

Post a Comment