Thursday, June 18, 2015

Mkutano Mkuu wa 2SEEDS Network 2015

 Hapa katika picha Wanamtandao wametawanyika katika vikundi mbalimbali wakijifunza mambo na hatua mbalimbali ambazo miradi imefikia kwa lengo la kubadilishana mawazo, kwa kuzingatia kuwa Mkutano mkuu kama huu ambao huwakutanisha Wanamtandao hawa hufanyika mara moja tuu katika mwaka.
 Wanamtandao wakiwa wamekusanyika katika Mradi wa Masoko (Masoko Project) wakiwa na shauku yakujua jinsi ambavyo shughuli ya ukusanyaji taarifa za bei na kuhifadhiwa katika mfumo wa Kompyuta wa Masoko yaani KMC Database System na baadaye kutumwa kwa wakulima na walaji wa bidhaa.
 Katika picha hapo juu ni Wajumbe  wa mkutano wakutoka katika miradi mbalimbali wakiwa wanamsikiliza Afisabiashara kutoka Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Vedastus Valentine akiwaelezea jambo kuhusu mradi wa Masoko ambao kazi yake kubwa ni kujenga Mfumo wa kuhifadhia na kutoa taarifa za bei kwa Wakulima na walaji wa bidhaa mbalimbali za mazao ambazo huuzwa katika Soko Kuu la Kariakoo.
Katika picha hapo juu ni Viongozi (Project Cordinators) wazawa  wa miradi yote nane inayoendelea kwa ushirikiano na Shirika la 2SEEDS Network lenye makao yake makuu  katika Jiji la Washington nchini Marekani. Katika miradi hiyo nane saba ipo katika vijiji vya Bombomajimoto,Kijungumoto,Magoma,Tabora,Kwakiliga,Magoma kwata ,Lutindi hii saba ipo Wilayani Korogwe na Mradi mmoja wa Masoko huu upo katika Soko Kuu la Kariakoo Jijini Dar Es Salaam.