Sunday, July 13, 2014

Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi

Wajumbe wa Mkutano wa Baraza la Shirika la Masoko wakiwa wanafuatilia taarifa zilizokuwa zikiendelea kutolewa katika mkutano huo wa baraza la Wafanyakazi uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika Ukumbi wa mikutano wa Shirika.
 Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Florens Seiya  akiongoza mkutano mkuu wa Baraza la Wafanyakazi mwishoni mwa wiki iliyopita.Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Shirika.Kwa kawaida mkutano huo mkuu huhudhuriwa na Mjumbe mmoja wa TUICO kutoka Tuico ngazi ya Mkoa.

Katika picha hapo juu ni Meneja Utumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Godwin Mrosso mwenye shati nyeupe na Mjumbe wa TUICO Mkoa Bwana Willy Kibona kwa pamoja wakiwa katika Ukumbi wa Mikutano walipokuwa wanahudhuria Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Shirika  la Masoko ya Kariakoo.