Tuesday, March 31, 2015

Samaki wa kila aina Sokoni Kariakoo

Kariakoo ni Soko kuu na kubwa sana hapa nchini Tanzania na hata katika Ukanda huu wa Afrika Mashariki.Hupokea mazao ya kila aina kutoka mikoani na hata nchi jirani. katika picha hapo juu ni samaki wakavu ambao hawa huingizwa hapa sokoni kutoka Mkoani Morogoro hasa wilaya za Kilombero na Ulanga. Ukifika Sokoni Kariakoo samaki hawa wakavu wanapatikana eneo la Shimoni soko la samaki na dagaa. Samaki wa maji baridi na chumvi wote wapo hapo. Karibuni nyote katika Soko la Kariakoo!

Bidhaa zaongezeka bei Sokoni Kariakoo

 Bei ya karoti ni kati ya Sh.1500/= hadi 1800/= kwa Kilo moja bei ya rejareja  na wakati  Pilipili hoho ni kati ya sh.1500/= hadi 1700/= kwa Kilo moja.
Msimu huu nyanya zimepungua kwa kiasi kikubwa ,hii ni kutokana hali ya hewa kwa sasa ni mvua nyingi zinanyesha mikoani  hivyo hata uzalishaji wake si mzuri. Kutokana na hali hiyo basi nyanya zimepanda bei kwa kiasi kikubwa! kwa kufikia sh.2000/= hadi 2500/= kwa kilo moja.