Monday, April 28, 2014

Sokoni Kariakoo Leo! Karibuniiii!

 Kijana huyu anaeonekana katika picha hapo juu alijitambulisha kwa jina  la Said Eyasi;  alikutwa mapema leo katika eneo la Soko la Jumla eneo la Shimoni. Alipohojiwa kuwa anafanya nini huko? Alijibu kuwa yeye anafanya biashara ya mifuko. Kijana huyu ana umri wa miaka 13 hivi sasa;hata alipoulizwa kuhusu shule, alijibu kuwa yeye alikwisha hitimu elimu ya msingi muda mrefu.