Wednesday, June 3, 2015

Watumishi wa Shirika la Masoko Kariakoo

 Katika picha hapo juu ni Bwana James Kanyilili akiwa ofisini kwake mapema leo asubuhi. Bwana Kanyilili ni mtumishi wa Shirika hili la Masoko katika Idara ya Fedha

Katika picha hapo juu ni Bwana Jacob Nombo,naye pia akiwa mezani anaendelea na shughuli zake za kila siku,naye ni mtumishi katika Idara ya Fedha.

KIKAO CHA BODI YA USHAURI

 Kikao cha Bodi ya Ushauri kilichofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita. Kikao hicho kilikuwa na kazi ya kujadili na kuipitisha Bajeti ya Shirika kwa mwaka wa fedha 2015/2016. Katika picha hapo juu kutoka kulia ni Bi.Sarah Yohana Kaimu Mwenyekiti wa Bodi akiongoza kikao hicho, wa pili  ni Katibu wa Bodi ambaye pia ni Meneja Mkuu wa Shirika Bwana Florens F.Seiya na anayefuata ni Meneja Utumishi wa Shirika Bwana Godwin Mrosso.

Katika picha hapo juu ni Bi.Sarah Yohana Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Shirika la Masoko Kariakoo,akifunga kikao cha Bodi hiyo mara baada ya kujadili na kuipitisha bajeti ya Shirika  kwa mwaka wa fedha wa 2015/2016 mwishoni mwa wiki iliyopita. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Shirika la Masoko Kariakoo.