Tuesday, November 24, 2015

Mboga aina zote Kariakoo Sokoni

Katika picha hapo juu ni mfanyabiashara wa mazao ya mbogamboga akiwa na mteja katika meza yake.Katika soko hili kila aina ya mbogamboga hupatikana takribani mwaka mzima!

SOKONI KARIAKOO

 Eneo la shimoni katika Soko Kuu la Kariakoo ambako bidhaa mbalimbali huuzwa kwa bei ya jumla na rejareja, eneo hili kwa sasa limekuwa bora zaidi kimpangilio kwa wafanyabiashara na kufanyiwa marekebisho ya taa za umeme ambazo zimeongeza mwanga wa kutosha.

 Nafaka za aina mbalimbali zinapatikana katika Soko Kuu la Kariakoo,ukifika sokoni utazipata nafaka hizi katika eneo la Soko dogo lililopo pembezoni mwa Jengo la Soko Kuu.

Katika picha akina mama hawa wakiwa Sokoni Kariakoo wakiandaa maharage mabichi kwa kuyamenya maganda  ili waweze kuwauzia wateja wao. Katika eneo hili kwa sasa limeboreshwa kwani sio tena wanakaa chini badala yake wanatumia meza nzuri na bora kwa kuhifadhia bidhaa zao wakati wa kuuza. Karibu sokoni Kariakoo.

Thursday, October 22, 2015

Mazao katika Soko Kuu la Kariakoo - Dar Es Salaam

 Zabibu ni miongoni mwa bidhaa zinazopatikana hapa Soko Kuu la Kariakoo, Jijini Dar Es Salaam. Bidhaa hii huzalishwa kwa wingi  mkoani Dodoma
vitunguu  saumu na tangawizi pia huuzwa katika soko kuu la Kariakoo. 
Pilipili Hoho hupatikana katika Soko kuu la Kariakoo takribani mwaka mzima. Pilipili hoho  huingizwa katika soko hili zikitokea katika mikoa mbalimbali ikiwemo Morogoro,Pwani na Tanga.Kwa bei ya jumla na rejareja huuzwa sokoni hapa kuanzia mapema alfajiri hadi jioni.

Monday, August 24, 2015

Matukio katika Picha

 Katika picha hapo juu kutoka kulia ni Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Florens Seiya, Mwenyekiti wa TUICO tawi Bwana Dennis Mfuruki aliyesimama na Bwana Henry Rwejuna ambaye ni Katibu wa TUICO tawi, kwa pamoja wakiwa wanaendesha mkutano wa wafanyakazi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo mwishoni mwa wiki iliyopita. Ni moja ya mikutano ya kawaida ambayo imekuwa inafanyika kwa nia ya kujenga na kuimarisha mahusiano baina wafanyakazi wa shirika na Mwajiri wao, wakilenga zaidi hali ya mwenendo mzima wa Shirika.
 katika picha hapo juu ni vitunguu maji ambavyo ni moja ya bidhaa zinazouzwa hapa katika soko  Kuu la Kariakoo jijini Dar Es Salaam.Vitunguu maji hivi hufikishwa sokoni Kariakoo vikiwa vinatoka mikoa mbalimbali ya Tanzania kama vile Mbeya,Arusha,Iringa na Singida.
Picha hiyo hapo juu inaonyesha sehemu tuu ya Watumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo wakiwa wametulia huku wakifuatilia maelezo ya Meneja Mkuu wa Shirika ,pichani hapo juu hayupo wakati wa mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Shirika mwishoni mwa wiki iliyopita.

Thursday, August 20, 2015

SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO



TANGAZO LA KAZI

Shirika la Masoko ya Karikaoo ni Shirika la Umma lililoanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Bunge Na.32 ya mwaka 1974 na kupewa majukumu ya kusimamia na kuendesha Soko Kuu la Kariakoo pamoja na Masoko mengine yatakayokuwa chini ya usimamizi wa Shirika pia kujenga Masoko mengine mapya katika Jiji la Dar es Salaam na kusimamia uendeshaji wake. Shirika linakaribisha maombi ya nafasi  mbili za kazi zifuatazo:
  1. Mwanasheria  Daraja la 11
Muombaji awe na Shahada ya Sheria kutoka Chuo Kikuu kinachotambuliwa na Serikali. Awe amepitia Shule ya Sheria na kusajiliwa kama Wakili.
Kazi na Majukumu.
Kushauri masuala ya kisheria katika Shirika la Masoko ya Kariakoo.
Kuandaa nyaraka zote za kisheria kwa ajili ya kusaidia kufikia malengo ya Shirika.
Kufuatilia na kutunza kumbukumbu muhimu kwa ajili ya kutumika kwenye mashauri Mahakamani.
Kuandaa mihutasari ya mashauri mbalimbali ya shirika yaliyopo mahakamani.
Kuandaa na kupeleka notisi za kisheria kwa wadaiwa wa shirika  .
Kufanya shughuli yeyote atakayo pangiwa na Meneja Mkuu au Mkuu wa kitengo.
  1. Ofisa Ugavi Msaidizi
Muombaji awe na Stashahada ya katika fani ya ununuzi na ugavi, awe amesajiliwa na PSPTB
Kazi na Majukumu.
Kuhakikisha kuwa vifaa vinavyonunuliwa vinapokelewa na kuingizwa katika vitabu vya Shirika..
Kuhakikisha kuwa nyaraka zote za stoo zinajazwa kwa ufasaha na kwa wakati.
Kuhakikisha kuwa mali zote zilizoifadhiwa stoo zinatuzwa  bila upotevu wowote.
Kuhakikisha kuwa uingizaji na utoaji wa bidhaa unafuata sheria na kanuni za manunuzi ya umma.
Kuhakikisha kuwa vifaa na mali zinazohifadhiwa stoo zinatunzwa katika mpangilio mzuri
Kufanya kazi zozote atakazopangiwa na Mkuu wa Kitengo.
MASHARTI YA JUMLA
Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45
 Waombaji wote waambatishe nakala ya cheti cha kuzaliwa. Na picha (passport size) moja ya rangi
Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
Maombi yote yaambatane na nakala za vyeti vya kidato cha nne na kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na nakala ya  vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.

Mwisho wa Kupokea maombi ni 29/08/2015.

Maombi hayo yatumwe kwa :

Meneja Mkuu,
Shirika la Masoko ya Kariakoo,
P.O.BOX 15789,
Dar es Salaam.
Na kwa Email: info@kariaakoo.or.tz.


Thursday, August 13, 2015

TANGAZO MAALUM



SHIRIKA LA MASOKO KARIAKOO
(KARIAKOO MARKETS CORPORATION)



AP/109/KMC/2015/2016/C

Expression of Interest



For

PROVISION OF CONSULTANCY SERVICES

Date: 10th August 2015
1.   The Kariakoo Markets Corporation has set aside funds towards the cost of providing consultancy services as described below and it intends to apply part of the proceeds of this fund to cover eligible payments under the contract.

S/N
TENDER DESCRIPTION
LOT/TENDER NUMBER
01
Preparation of Strategic plan (2015 – 2018)
PA/109/2015/2016/STP/C/01
02
Valuation of Assets
PA/109/2015/2016/VA/C/01

2.   The Kariakoo Markets Corporation now invites eligible registered Local Consultancy firms to indicate their interests in providing the services mentioned above.

3.   Interested individual consultants must provide information indicating that they are qualified to perform the services by submitting consultant’s profile, description of similar assignments, experience in similar conditions, availability of appropriate skills among staff, etc.

4.   A consultant will be selected in accordance with the procedures set out in the Public Procurement Act 2011 and the Public Procurement Regulations – Government Notice No. 466 of 2013.

5.   Interested eligible consultants may obtain further information from the office of the Tender Board Secretary, Kariakoo Markets Corporation, P.o.Box 15789, Dar es Salaam from 08:30am to 03:30 pm on Monday to Friday inclusive except on public holidays.

6.   Expressions of Interest (EoI) must be delivered to the address below not more than 25thAugust 2015 at or before 10:00hrs.

The Secretary,
Kariakoo Markets Corporation Tender Board,
P.o.Box 15789,
Dar es Salaam.

7.   Closing date for receiving the expression of interest is 25thAugust 2015 at 10:00. Late Expressions of Interest shall not be accepted for evaluation irrespective of the circumstances.



General Manager
Kariakoo Market Corporation

WANAMTANDAO WA LUTINDI-KOROGWE

Miongoni mwa miradi ambayo imepata mafanikio makubwa inayosimamiwa na 2SEEDS Network wilayani Korogwe Vijijini ni ule uliopo katika kijiji cha Lutindi. Mradi huu unastawisha mazao ya mbogamboga kama vile inavyoonekana katika picha hapo juu shamba la moga aina ya kabichi linavyoendelea kutunzwa na wanakikundi.Mbali na mboga aina ya kabichi pia wanazalisha pilipili hoho,bitroots,bilinganya na nyanya chungu.

Sunday, June 28, 2015

Soko Kuu Kariakoo Na Wakulima Vijijini

 Soko Kuu la Kariakoo haliishii tuu kupokea mazao yanayofika Sokoni badala yake sasa limekuwa likifanya ziara maalumu kuwatembelea wakulima walioko vijijini hasa katika Wilaya ya Korogwe kwa kuanzia, huku wakishirikiana na 2SEEDS Network shirika lisilokuwa la Kiserikali kutoka nchini Marekani kwa pamoja taasisi hizi mbili zimekuwa zikiwasaidia wakulima katika kuibua na kuendesha miradi mbalimbali ya kiuzalishaji mali, pia Soko  la Kariakoo likiwapa msaada zaidi kwakuwapa kipaumbele katika kupata soko la mazao wanayozalisha. Katika picha hapo juu ni moja ya mashamba ya wakulima hao walioko Korogwe Vijijini.

 Katika picha hapo juu ni Wanamtandao wa 2SEEDS Network wakiwa shambani wakiangalia maandalizi ya shamba yakiendelea. Mratibu wa mradi huo Bwana Cameron mwenye begi mgongoni alifika kijijini Bungu

Katika picha hapo juu ni shamba la mboga aina ya kabichi, shamba hili lipo katika kijiji cha Lutindi juu milimani kabisa Korogwe Vijijini. Mazao haya kwa kiasi kikubwa husafirishwa kuja  kuuzwa katika Soko kuu la Kariakoo Jijini Dar Es Salaam. Kwa ushirikiano wa 2SEEDS Network wakulima hawa wamekuwa wakizalisha kwa bidii mazao mbalimbali kama vile pilipili hoho,karoti,vitunguu maji, conflowers,bitroots n.k

Thursday, June 18, 2015

Mkutano Mkuu wa 2SEEDS Network 2015

 Hapa katika picha Wanamtandao wametawanyika katika vikundi mbalimbali wakijifunza mambo na hatua mbalimbali ambazo miradi imefikia kwa lengo la kubadilishana mawazo, kwa kuzingatia kuwa Mkutano mkuu kama huu ambao huwakutanisha Wanamtandao hawa hufanyika mara moja tuu katika mwaka.
 Wanamtandao wakiwa wamekusanyika katika Mradi wa Masoko (Masoko Project) wakiwa na shauku yakujua jinsi ambavyo shughuli ya ukusanyaji taarifa za bei na kuhifadhiwa katika mfumo wa Kompyuta wa Masoko yaani KMC Database System na baadaye kutumwa kwa wakulima na walaji wa bidhaa.
 Katika picha hapo juu ni Wajumbe  wa mkutano wakutoka katika miradi mbalimbali wakiwa wanamsikiliza Afisabiashara kutoka Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Vedastus Valentine akiwaelezea jambo kuhusu mradi wa Masoko ambao kazi yake kubwa ni kujenga Mfumo wa kuhifadhia na kutoa taarifa za bei kwa Wakulima na walaji wa bidhaa mbalimbali za mazao ambazo huuzwa katika Soko Kuu la Kariakoo.
Katika picha hapo juu ni Viongozi (Project Cordinators) wazawa  wa miradi yote nane inayoendelea kwa ushirikiano na Shirika la 2SEEDS Network lenye makao yake makuu  katika Jiji la Washington nchini Marekani. Katika miradi hiyo nane saba ipo katika vijiji vya Bombomajimoto,Kijungumoto,Magoma,Tabora,Kwakiliga,Magoma kwata ,Lutindi hii saba ipo Wilayani Korogwe na Mradi mmoja wa Masoko huu upo katika Soko Kuu la Kariakoo Jijini Dar Es Salaam.

Tuesday, June 16, 2015

Miradi ya Wanamtandao wa 2SEEDS Network

 Katika picha hapo juu ni Wanamtandao wa 2SEEDS Network,akina mama hawa wamekuwa wakijituma kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha wanafikia malengo yao ya Kikundi. Wanamtandao hawa wapo katika Kijiji cha Tabora nje kidogo ya Wilaya ya Korogwe.Wanamtandao wanajishughulisha na utengenezaji wa Crips za viazi,karanga zenye mchanganyiko na mayai na wanakausha mboga za majani kwa kutumia mashine za bei nafuu, amabayo kila mwanamtandao katika kikundi anamiliki.
Mradi katika picha hapo juu unavyojaribu kuelezea malengo ya miradi yote ni kuwabadilisha maisha yao Wanamtandao.
Kijungumoto mradi pekee miongoni mwa miradi nane, wenye kutoa asali na nta na umekuwa wenye mafanikio makubwa sasa tangu umeanzishwa na tayari Wanamtandao wameanza kufaidi matunda yake.

Monday, June 15, 2015

Mradi wa Vitunguu saum- Bombo Majimoto Korogwe

Picha ya hapo juu inaonyesha mojawapo ya Nyumba za mazao(Green House) ambazo ndani yake kama unavyoweza kuona mna matuta kadhaa ya vitunguu saum.Mradi huu umeonekana kuwa wenye kuleta mafanikio makubwa kwa wanakikundi cha Bombomajimoto,ambapo mbali ya shamba hili la pamoja tayari kila mwanakikundi ameanzisha shamba lake binafsi ili aweze kustawisha zao hili la vitunguu saum.

 Katika picha hapo juu ni sehemu tuu ya  matuta katika shamba la  vitunguu saum vinavyoendelea kustawishwa na wanakikundi hiki cha Bombomajimoto huko Korogwe Vijijini chini ya uangalizi wa Shirika la 2Seeds Network.

 Katika picha hapo juu ni kabati ambalo linatumiwa na Wanakikundi  cha BomboMajimoto kutunzia vifaa mbalimbali yakiwemo madawa maalum kwa ajili ya kutunza mazao katika mashamba yao.
 Hapo juu ni picha ya pamoja ya Wanakikundi wa Bombo Majimoto na wageni waliowatembelea kuona maendeleo ya mradi wa vitunguu saum unaoendeshwa kwa njia ya kilimo cha kawaida na kwakutumia mfumo wa nyumba za mazao(Green house). Kutoka kushoto ni Bwana Anderson Shaka Mtaalamu wa Mawasiliano kwa njia ya Kompyuta  kutoka Shirika la Masoko Kariakoo, wapili ni Mama Tatu Mwanakikundi, Bwana Vedastus Valentine Afisa Biashara kutoka Shirika la Masoko Kariakoo, Bwana Shebe mwanakikundi  ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kikundi na aliyekaa ni Bwana Hamdani naye ni Mwanakikundi.
Afisa biashara wa Shirika la Masoko Kariakoo aliyesimama katikati Bwana Vedastus Valentine akiwapa ushauri Wanamtandao wa 2Seeds Network wa kikundi cha Bombo Majimoto Korogwe Vijijini wakati alipowatembelea ili kujionea maendeleo ya mradi huo wa vitunguu saum.wengine waliosimama aliyevaa kofia ni Bwana Shebe ambaye ni mwenyekiti wa Kikundi cha mradi huo na mwingine ni Bwana Hamdani.

Wednesday, June 10, 2015

Wanamtandao

Katika picha hapo juu ni ya Wanamtandao amabao wameunganishwa na Shirika la 2SEEDS Network ambao wamo katika vikundi tofautitofauti kutoka katika miradi mbalimbali ipatayo nane na ambayo imesambaa katika vijiji mbalimbali vilivyomo katika wilaya ya Korogwe Vijijini. Vijiji hivyo ni hivi vifuatavyo Kwakiliga,Tabora,Magoma, Magoma Kwata, Bombo Majimoto,Kijungumoto,Lutindi na Bungu.

Katika vijiji hivyo kuna miradi mbalimbali ya uzalishaji mali kama vile ufugaji nyuki,kuku na mbuzi na kilimo cha mazao mbalimbali.

Tutakuwa tunawaletea taarifa za mradi mmojammoja kila siku hadi mwisho.

Wanamtandao wa 2SEEDS Network - Korogwe Vijijini

 Katika picha hapo juu ni sehemu ya bwawa la samaki, na banda la kuku ambalo limejengwa ndani ya eneo la bwawa kama linavyoonekana hapo katika picha. Miradi hii miwili inategemeana kiutunzaji kwani mbolea inayotokana na kuku katika banda hudondokea ndani ya bwawa la samaki na kuwa chakula cha samaki. Miradi hii ipo katika kijiji cha Magoma Kwata wilayani Korogwe vijijini,lakini pia miradi hii iliyobuniwa na Wanamtandao wa 2Seeds Network ipo chini ya uangalizi wanamtandao wa Shule ya Msingi Kwata.

 Katika picha hapo juu ni banda la kuku likwa na kuku ndani yake na tayari mradi huu umeanza kuzalisha mayai,mojawapo ya miradi iliyopo katika Kijiji cha Magoma Kwata unaosimamiwa na baadhi ya Wanafunzi wa Shule hiyo ya Kwata ambao wameunganishwa katika Mtandao wa 2SEEDS Network.

 Katika picha hapo juu ni mradi wa Vitunguu saumu ambao naoupo katika kijiji cha Magoma Kwata,wanamtandao waliopo katika kikundi hiki hutumia drip irrigation method katika kumwagilia mimea ya vitunguu katika matuta yake kama inavyoonekana mipira hiyo midogomidogo imetandazwa kwa kufuata mistari ya mimea.

 Katika picha hapo juu aliyesimama wapili kutoka kulia ni Bwana Vedastus Valentine ambaye ni Afisa Biashara kutoka Shirika la Masoko Kariakoo akiwa anamsikiliza mwanakikundi anaejulikana kwa jina Babu Francis  Mwamkai aliyeshika miwani mkononi mwake akitoa maelezo jinsi wanavyojitahidi kuenedesha miradi yao kwa umakini ili waweze kufikia malengo yakufikia maisha bora.

Katika picha hapo juu ni Mradi wa mbuzi wa maziwa ambao pia upo katika Kijiji hichohicho cha Magoma Kwata, tayari mradi huu umeanza kutoa matunda kwakutoa maziwa. maziwa hayo yanatumiwa na wanafunzi katika kuboresha afya zao,lakini kwa mujibu wa maelezo ya babu Francis Mwamkai wanao mpango wa kuongeza idadi ya mbuzi hao katika kuhakikisha kuwa mradi huo unawaletea tija zaidi.