Tuesday, November 24, 2015

Mboga aina zote Kariakoo Sokoni

Katika picha hapo juu ni mfanyabiashara wa mazao ya mbogamboga akiwa na mteja katika meza yake.Katika soko hili kila aina ya mbogamboga hupatikana takribani mwaka mzima!

SOKONI KARIAKOO

 Eneo la shimoni katika Soko Kuu la Kariakoo ambako bidhaa mbalimbali huuzwa kwa bei ya jumla na rejareja, eneo hili kwa sasa limekuwa bora zaidi kimpangilio kwa wafanyabiashara na kufanyiwa marekebisho ya taa za umeme ambazo zimeongeza mwanga wa kutosha.

 Nafaka za aina mbalimbali zinapatikana katika Soko Kuu la Kariakoo,ukifika sokoni utazipata nafaka hizi katika eneo la Soko dogo lililopo pembezoni mwa Jengo la Soko Kuu.

Katika picha akina mama hawa wakiwa Sokoni Kariakoo wakiandaa maharage mabichi kwa kuyamenya maganda  ili waweze kuwauzia wateja wao. Katika eneo hili kwa sasa limeboreshwa kwani sio tena wanakaa chini badala yake wanatumia meza nzuri na bora kwa kuhifadhia bidhaa zao wakati wa kuuza. Karibu sokoni Kariakoo.