Monday, June 23, 2014

Shirika la Masoko ya Kariakoo pamoja na Washirika wake 2Seeds Network na Habari Mazao


Kariakoo Market Corporation (KMC) na Washirika wake 2Seeds Network na Habari Mazao
kwa pamoja watafanya uzinduzi wa Tovuti,Blog na Huduma ya SMS.
Huduma ya SMS (SMS SOLUTION) inatarajiwa kutumiwa katika kutoa taarifa za bei za mazao mbalimbali ambayo huletwa katika Soko Kuu la Kariakoo lililopo Jijini Dar Es Salaam. Vyombo kadhaa vya Habari vimealikwa katika Uzinduzi huo kesho tarehe 24/6/2014 kuanzia saa 4.00  hadi 4.30 asubuhi.
Hafla hiyo itafanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Shirika la Masoko ya Kariakoo uliopo katika Jengo Kuu la Soko ghorofa ya Kwanza.