Monday, May 26, 2014

Kutoka Sokoni Kariakoo leo!

 Karoti na Pilipili Hoho pamoja na mboga  mbalimbali  za majani hupatikana katika Soko kuu la Kariakoo kwa wingi sana kila siku. Lakini bidha hizi zote zipo katika viwango vya hali ya juu katika ubora kwa mlaji kwa kuzingatia mazingira bora ya Soko la Kariakoo llilopo hapa Jijini Dar es Salaam-Tanzania.
Nyanya kutoka Iringa zinaingia katika Soko Kuu la Kariakoo kila siku katika majira haya. Nyanya hizi kutoka mkoani Iringa huanza msimu wa mwezi Mei na kuendelea; zina ubora wa kipekeee sana katika matumizi.Sasa usikose kujipatia bidhaa hii bora fika Kariakoo Sokoni eneo la Shimoni ambapo utaweza kupata kwa bei ya jumula na rejareja kwa kadiri ya mahitaji yako iwe ya familia au biashara. Karibu sanaaaa!

No comments:

Post a Comment