Sunday, December 14, 2014

Bidhaa za vyakula sokoni Kariakoo

 Karoti nzuri daraja la kwanza kabisa kutoka Mikoa mbalimbali ya Tanzania.Karibu ujipatie bidhaa hii bora kwa matumizi mbalimbali kama vile kutengeneza juice na nakadhalika.
Katika picha hapo juu ni Viazi mviringo vikiwa bado fresh kabisa kutoka mkoani. Mikoa mashuhuri kwa uzalishaji vyazi hapa nchini ni pamoja na Iringa,Njombe na Mbeya

Tuesday, December 9, 2014

Kuelekea Sikukuu za Christmas na Mwaka mpya!

 Njegere ni moja ya bidhaa adimu na yenye kupendwa sana na watu wengi kwa matumizi ya chakula. Njegere huingia katika Soko Kuu la Kariakoo kutoka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania kama vile Morogoro,Iringa,Njombe na kwingineko. Bidhaa hii kuelekea sikukuu za Christmas na Mwaka mpya bado inapatikana kwa wingi hapa Sokoni  hasa eneo la Shimoni.katika picha hapo juu Mfanyabiashara alikutwa na mpiga picha akiwa amekwisha kuzimenya njegere zake tayari kwa kuwauzia wateja mbalimbali.

Sokoni Kariakoo kuna kila aina ya vyakula.Katika picha hapo juu nafaka mbalimbali ambazo huuzwa katika soko Dogo.Mfanya biashara huyu ameweka wazi hata bei za vyakula kwa kuzingatia madaraja au ubora wake.Tunapoelekea katika Sikukuu za mwisho wa mwaka bei za vyakula hazijabadilika sana! Karibuni Sokoni kwa manunuzi ya bidhaa mbalimbali.

Thursday, December 4, 2014

Watumishi KMC

 Katika picha hapo juu ni Meneja Utumishi na Uendeshaji  Bwana Godwin Mrosso akiwa pamoja na  Mkuu  wa Kitengo cha Usalama Bwana Josam Mnzava.  Wote ni Watumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo.
Katika picha hapo juu ni Mkaguzi Mkuu wa Shirika Bwana Paul Kiwera  akiwa anabadilishana mawazo na Mwanasheria wa Shirika Bibi.Gloria Kalabamu muda mfupi kabla ya kikao cha Bodi.kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa mikutano wa  Shirika la Masoko ya Kariakoo.

Tuesday, October 28, 2014

Mkutano wa Bodi ya Ushauri ya Shirika la Masoko Kariakoo

 Katika picha hapo juu ni Wajumbe wa Mkutano wa Bodi ya Ushauri ya Shirika la Masoko ya Kariakoo wakiwa wanatoka kwenda kupanda basi maalumu lililokuwa  limekodiwa kwa ajili ya kwenda kutembelea na kukagua mali za Shirika. Aliyetangulia mbele ni Meneja Mkuu wa Shirika Bwana Florens Seiya na anayefuata ni Mwenyekiti wa Bodi Bwana Wilson Kabwe.Hii ilikuwa ni mojawapo ya agenda za kikao hicho cha Bodi.
 Miongoni mwa Wajumbe waliohudhuria Mkutano wa  Bodi ya Ushauri wakipanda basi tayari kwa safari kuelekea maeneo ya Mbezi Beach ambako ziko nyumba za Shirika la Masoko ya Kariakoo, mwishoni mwa wiki iliyopita.
 Wajumbe wa Mkutano wa Bodi ya Ushauri wakiwa wamefika mahali zilipo nyumba za Shirika la Masoko ya Kariakoo.Katika picha Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bwana Wilson Kabwe akiwasalimia Wajumbe wa Mkutano huo.
 Wajumbe wa mkutano wa Bodi wakitembea kuelekea katika geti la nyumba mojawapo eneo la Mbezi Beach Makonde, huku wakiongozwa mbele na Afisa Usalama Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Josam Mnzava ambaye ameshikilia radio Call.
 Wajumbe wa Mkutano wa Bodi ya Ushauri ya Shirika wakiwa nje ya geti la nyumba mojawapo ya Shirika la Masoko Kariakoo,nyumba hizi zipo eneo la Mbezi Beach Mtaa wa Makonde.Anaye toa maelezo hapo ni Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Florens Seiya.Hii ilikuwa ni mwishoni mwa wiki liyopita.
 Wajumbe wa Bodi ya ushauri walipata nafasi ya kutembelea na kukagua mali zinazomilikiwa na Shirika la Masoko ya Kariakoo.Hapo juu katika picha ni wajumbe hao walipokuwa eneo la Tabata bima Jijini Dar Es Salaam, ambako walifika kuona nyumba za Shirika hilo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Wilson Kabwe ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Jiji la Dar Es Salaam.Katika picha alikuwa akifungua Mkutano wa Bodi  mwishoni mwa wiki iliyopita.Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Shirika la Masoko ya Kariakoo.

Monday, October 20, 2014

Wafanyabiashara wa Soko Kuu la kariakoo

Katika picha hapo juu ni miongoni mwa Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kariakoo wakiwa katika moja ya Masoko ya nje ambayo hufanyika Osterbay na Masaki jijini Dar Es Salaam siku za Jumamosi na Jumapili.Lakini pia katika Masoko haya huwashirikisha wakulima kutoka Wilaya ya Korogwe ambao husimamiwa miradi yao ya uzalishaji mali na matandao wa 2SEEDS Network.

Monday, October 13, 2014

Miongoni mwa Tunu za Hayati Baba wa Taifa Mwl.Julius K.Nyerere ambazo zingali zinaishi hadi leo!

 Ni miaka 15 tangu Baba wa Taifa alipotutoka Watanzania na Ulimwengu kwa ujumla,lakini angali anaishi pamoja na Watanzania wa aina zote.Shirika la Masoko Kariakoo ni mojawapo ya Mashirika yaliyoanzishwa wakati wa uongozi wake mnamo mwaka 1974 kwa sheria ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.Soko Kuu la Kariakoo lilianzishwa maalum kwa ajili ya  Watanzania hasa wakulima na Wafanyabiashara wadogowadogo waendeshe shughuli zao hapa ili kuwakomboa kimaendeleo.Mwalimu alimjali kila mwananchi kwa nafasi yake.

 Katika picha hapo juu ni Soko Kuu la Kariakoo katika mwaka wa 1975 mara baada ya kufunguliwa rasmi na Baba wa Taifa Hayati Mwl.Julius K. Nyerere.Wakati huu Soko Kuu la kariakoo lilikuwa na Wafanyabiashara kati ya 200 hadi 300, ambao walikuwa wakifanya biashara zao hapa.

 Hii ilikuwa ni tarehe 8/12/1975 Hayati  Mwalimu Julius K.Nyerere wakati huo akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaonekana akikata utepe kama ishara ya kufungua rasmi Jengo la Soko Kuu la Kariakoo.Ujenzi wake uligharimu kiasi cha Shilingi 22,000,000/=fedha za Kitanzania na pia lilijengwa na Wakandarasi wazawa tangu uchoraji na usanifu wa ramani kazi ambayo ilifanywa na Mhandisi Mzee wetu Beda Amuli nakujengwa na Kampuni ya MECCO kwa wakati. Jengo hili kwa sasa linakadiriwa kuwa na thamani ya Sh.Bilioni 50.

Picha hii hapo juu inaonyesha watumiaji wa Soko Kuu la Kariakoo wakiwa wameongeza sana, hii ni miaka ya hivi karibuni. Wananchi wengi wakiwa wamejaa kupata mahitaji mbalimbali.

Tutakukumbuka daima kwani umetuachia Tunu za kila aina katika Taifa hili.

Friday, September 26, 2014

Mama Majasiriamali


Mama huyu katika picha hufanya biashara ya dagaa katika Soko Kuu la Kariakoo. Mezani kwake kuna kila aina ya dagaa ambao huwauza.Mama huyu yupo eneo la Wauza dagaa na samaki katika eneo la Shimoni.Katika alikutwa akiwapimia wateja wake dagaa!

Sokoni Kariakoo leo!

 Hawa ni samaki aina ya Sangara kutoka Ziwa Victoria. Samaki hao wameshakaangwa safi tayari kabisa kwa matumizi ya mboga! Ukiwa katika Soko la Kariakoo ingia eneo Shimoni kwenye eneo la biashara ya samaki utawapata.Karibuniii!
Pichani hapo juu ni aina mojawapo ya mboga za majani zinazopatikana katika soko Kuu la Kariakoo; mboga hiyo huuzwa kwa kilo kati ya Sh.1000/= hadi 1500/=. Fika eneo la Shimoni utazipata mboga hizi na nyinginezo pia!

Sunday, September 21, 2014

Ndizi kutoka Morogoro

Ndizi aina hii kwa wakati huu zinatoka Mkoani Morogoro hasa katika wilaya ya Kilombero katika kijiji maarufu kiitwacho Mbingu. Kijiji hiki kinapitiwa na barabara inayounganisha mji wa Ifakara na Mlimba.Ndizi Mzuzu huzalishwa kwa wingi sana katika kijiji hiki.

Tuesday, September 16, 2014

Kariakoo leo

 Katika picha hapo juu ni Wajasiriamali ambao hufanya shughuli zao za kutengeneza mifuk/vifungashio vya bidhaa ndogondogo kama vile viungo vya vyakula,karanga, bisi nakadhalika katika ukubwa wa aina tofautitofauti.Wajasiriamali hawa wapo katika moja vyumba vya Soko Dogo la Kariakoo Jijini Dar Es Salaam.Kwa mahitaji yako ya vifungashio hivi Sokoni Kariakoo katika Jengo la Soko Dogo
 Katika picha hapo juu ni moja ya Wateja waliofika katika sehemu hii ya Wajasiriamali wanaotengeneza vifungashio vya mifuko ya nailoni ili kununua.Vifungashio hivi hutengenezwa kwa kutmia mashine ndogondogo ambazo huendeshwa kwa mkono na zingine hutumia nishati ndogo ya umeme.
Sokoni Kariakoo kuna mpangilio mzuri wa kila jambo;katika picha hapo juu ni magari ya Wateja mbalimbali ambao wamefika kujipatia mahitaji katika Soko Kuu la Kariakoo.Magari haya yapo katika hali ya usalama bila shaka yoyote! hapo ni Mtaa wa Tandamti.

Monday, September 15, 2014

Kutoka Soko Kuu la Kariakoo - DSM

 Kitu gani ambacho ukifika katika Soko Kuu la Kariakoo hutakipataaaa? La hasha kuanzia nafaka,matunda,mboga mboga za majani hadi viungo vya kila aina.Katika picha hapo juu utaona Vitunguu swaum,Tangawizi,Ndimu na vinginevyo vipo kwa wingi mezani vikiwa katika ubora sana.Karibu Soko kuu la Kariakoo ujipatie bidhaa za kila aina. Bei ya vitunguu swaum na tangawizi ni kati ya Sh.4000 hadi 4500 kwa kilo moja.

 Miongoni mwa Watumishi wa Shirika la masoko ya Kariakoo ni Bwana Idd Mrope ambaye anaonekana katika picha hapo juu.Hapa yupo katika maeneo ya Ofisi za Shirika zilizopo katika ghorofa ya kwanza katika jengo la Soko Kuu.
Soko Kuu la Kariakoo ni Soko kubwa kuliko hapa nchini Tanzani,hii picha inaonesha sehemu mojawapo ya soko hili ambapo hapa barabara inayoingia katika eneo la soko la Jumla maarufu kama Shimoni.Eneo hili linaloonekana katika picha ni Geti Namba. 5 ambapo bidhaa karibu zote ambazo huingia hapa Sokoni hupitia hapa.

Friday, September 12, 2014

Matunda soko kuu kariakoo

 Picha ya zabibu kama inavyoonekana hapo juu katika Soko la Kariakoo leo ilikuwa ikiuza kwa bei ya shillingi elfu mbili mia tano kwa kilogram  na shillingi elfu thelathini kwa jumla


Katika picha hapo juu ni matunda aina ya ambazo kwa kiasi kikubwa huingizwa katika soko kuu la Kariakoo kila siku kutoka  mikoani na hususani katika mkoa Morogoro zinauzwa kwa bei  ya rejareja na jumla




Saturday, September 6, 2014

Hafla ya kukabidhi vyeti kwa Wafanyakazi bora

 Katika picha hapo juu ni Meneja Utumishi na Uendeshaji katika Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Godwin Mrosso anayepiga makofi mara baada ya kumkabidhi cheti maalum cha ufanyakazi bora Bibi Romana Lukanga  aliyeshika cheti,na aliyesimama katikati ni Bwana Joseph Mweyo ambaye ni Mwenyekiti wa TUICO katika Shirika la Masoko; na ambaye ameshika bahasha kulia kabisa ni Bibi Ester Chogero yeye ni Katibu wa TUICO hapa katika Shirika la Masoko.Meneja Utumishi alimuwakilisha Meneja Mkuu wa Shirika Bwana Florens Seiya ambaye alikuwa na shughuli zingine za kiofisi.Hafla hiyo ilifanyika jana mchana katika Ukumbi wa mikutano wa Shirika.
 Katika picha hapo juu ni Bibi Primitiva  Kamugisha  Kaimu Meneja wa Idara ya Usafi akipokea cheti cha Ufanyakazi bora kwa niaba ya Mtumishi wa Idara yake ambaye hakuwepo katika hafla hiyo hapo jana.
 Aliyesimama ni Bibi Romana Lukanga akitoa shukrani kwa Uongozi wa Shirika  kwa niaba ya Wafanayakazi bora waliotunukiwa vyeti,pamoja na shukrani lakini pia aliwasisitiza wafanyakazi wenzake waliopata vyeti hivyo kuwa wasibweteke nakuona kuwa wameshashinda bali inawapasa kuongeza bidii katika utendaji wao wa kazi ili wazidi kuwa mfano mara kwa mara katika Shirika.
 Katika picha hapo juu aliyesimama ni Meneja wa fedha katika Shirika la Masoko Mrs.Marieta Massaua akitoa  pongezi kwa Watumishi wa Shirika walioshinda na kuwa Wafanyakazi bora katika Shirika.Hafla hiyo iliyofanyika jana mchana katika Ukumbi wa Mikutano wa Shirika.
Bwana Ibrahim Masha akiwa amesimama kutoa nasaha kwa Watumishi wa Shirika waliohudhuria hafla ya kukabidhi vyeti kwa Wafanyakazi bora wa Shirika kwa mwaka 2012/2013.Hafla hiyo ilifanyika jana mchana katika Ukumbi wa Mikutano wa Shirika. Bwana Ibrahim Masha yeye ni Mjumbe wa halmashauri ya TUICO ngazi ya Taifa.

Thursday, September 4, 2014

Coneflowers & Salad

Coneflowers na Salad ni miongoni mwa mbogamboga ambazo hufikishwa sokoni Kariakoo kila siku.
Mboga hizi zinazalishwa mikoa ya Morogoro,Tanga na Arusha kwa  hapa Tanzania.
Karibu upate mbogamboga zilizo "fresh"

Wednesday, September 3, 2014

Matunda katika Soko Kuu la Kariakoo


 Aina hii ya maembe ni nzuri sana kwa kuandaa juisi na matumizi mengineyo! mahali pazuri yanapopatikana kwa bei nzuri ni katika Soko kuu la Kariakoo. Kwa bei ya jumla na rejareja utapata bila taabu! Katika soko hili maarufu kila aina ya matunda hupatikana muda wote katika mwaka!Fika eneo la Shimoni katika eneo la matunda.Karibu sanaa!


Tuesday, September 2, 2014

Nyanya Bora zinapatikana Soko Kuu la Kariakoo

 Katika picha hapo juu ni Mama Mjasiriamali ambaye alijitambulisha kwa jina la Mama Shakila; Mama huyu hufanya biashara ya nyanya katika Soko Kuu la Kariakoo eneo la Shimoni kuanzia mapema asubuhi hadi jioni.Katika mahojiano aliniambia nyanya hizi kwa majira haya zinatoka mkoani Morogoro.
Sokoni Kariakoo ni mahali pekee amabapo unaweza kupata bidhaa bora na ambazo zinaweza kukidhi mahitaji yako ya kila siku kwa bei ya wastani.Kama katika picha hapo juu nyanya nzuri amabazo zipo katika kiwango safi cha ubora zinapatikana hapa sokoni. Ukifika Kariakoo tunakukaribisha katika eneo la Soko la jumula na rejareja eneo la Shimoni. Nyanya ni moja bidhaa kadhaa ambazo husafirishwa kwenda katika visiwa vya Commoro. Karibuni mjipatie bidhaa hizi bora!

Tuesday, August 26, 2014

Usafi katika Soko Kuu la Kariakoo-Dar Es Salaam

Katika picha hapo juu ni Mtumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Amiri Magala akiwa anaendelea na shughuli yake ya kusafisha moja ya mifereji ya maji taka iliyopo eneo la Shimoni. Uongozi wa Shirika huzingatia sanaa suala zima la Usafi katika maeneo yote ya Soko Kuu la Kariakoo ambalo ni maarufu sana kwa kupokea bidhaa mbalimbali za mazao kutoka mikoani.Kwa kuzingatia hilo mifereji hii ya maji taka  hukaguliwa mara kwa mara kila siku ili kuhakikisha maji taka yanatoka na kuingia katika mfumo mkuu wa Jiji wa maji taka.

LEEKS ni nini?

Kwa wale wataalam wa mapishi na vyakula hawataweza kushangaa sana kuwa majani haya ni ya nini?au majani gani?
Hii ni mojawapo yambogamboga za majani za kisasa zinazoitwa LEEKS hizi hupatikana pia hapa sokoni Kariakoo kwa wingi sanaa! Fika Sokoni Kariakoo eneo la Shimoni katika meza za mbogamboga! zikiwa bado fresh utazipata! Karibu sanaaaa!

ZUKIN na BLUKOLIN

Katika picha hapo juu sio matango; ila ni moja ya mboga aina ya ZUKIN na BLUKOLIN.Aina hzi za mbogamboga huzalishwa kwa wingi katika mikoa ifuatayo; Morogoro,Tanga  katika wilaya za  Lushoto,Korogwe  na  kule Arusha.Fika Sokoni Kariakoo eneo la Shimoni utazipata kwa wingi na bei yake ni nzuri. Karibuni sana!

Saturday, August 23, 2014

Shughuli za biashara sokoni Kariakoo

Shughuli za biashara mbalimbali huendelea katika Soko Kuu la Kariakoo kila siku huanza  tangu mapema  alfajiri.Hapo katika picha wafanyabiashara wa matunda wakiwa katika eneo lao la biashara.Matunda mengi huuzwa eneo la Shimoni kwa bei ya rejareja na jumla pia.

Thursday, August 21, 2014

Usalama katika Soko Kuu la Kariakoo umezidi kuimarishwa

Katika Soko Kuu la Kariakoo lililopo Jijini Dar Es Salaam usalama kwa Wafanyabiashara na Wateja mbalimbali wanaofika kujipatia mahitaji mbalimbali umezidi kuimarishwa kwa kiasi kikubwa sana. Katika picha hapo juu ni Geti lakutokea soko la jumla lililopo sehemu ya Shimoni; askari akiwa getini kabisa hapo akifanya ukaguzi kwa kila anayepita kuingia au kutoka ndani ya soko.
Tunamkukaribisha kila mmoja  Sokoni Kariakoo.


Thursday, August 14, 2014

Habari toka Soko Kuu la Kariakoo leo!

Mazao ya  mbogamboga na Viungo yanapatikana kwa wingi sana katika soko Kuu la Kariakoo.Kama uonavyo katika picha hiyo hapo juu  ni baadhi tuu ya mazao ambayo huingia Sokoni kila siku .
 Dagaa hawa maalum wanaopatikana katika Ziwa Nyasa lililopo Kusini Magharibi mwa Tanzania;wana ladha ya kipekee sana wanapatikana pia katika Soko hili kubwa la Kariakoo eneo la Shimoni sehemu ya Wafanyabiashara wa dagaa.Karibuni mjipatie bidhaa hii muhim kwa afya ya familia yako.
 Shughuli za biashara katika Soko Kuu la Kariakoo hapa Jijini Dar es Salaam huanza mapema sana alfajiri kila siku.Hapa katika picha utaona Wafanyabiashara wa matunda mbalimbali wakiwa eneo la Shimoni wakiendelea na shughuli zao  za kibiashara kama walivyokutwa mapema alfajiri majira ya saa 11.30.
Magunia ya vitunguu yakiwa yamepangwa katika eneo la Soko la Jumla Shimoni Kariakoo Jijini  Dar Es Salaam.Vitunguu hivi majira haya vinatoka katika mikoa tofautitofauti ikiwamo Morogoro,Mbeya,Iringa na Dodoma pia.

Sunday, July 27, 2014

Maandalizi ya Sikukuu ya Idd katika mitaa ya Kariakoo

Watu mbalimbali Watanzania na wale wakutoka nchi jirani wakiwa katika pilikapilika za maandalizi ya sikukuu ya Idd.Maduka mengi yakiwa na bidhaa nyingi  mbalimbali ambazo zimekuwa na bei za wastani kama vile baadhi ya Wananchi walivyotoa maoni yao  mwishoni mwa wiki iliyopita.

Friday, July 25, 2014

KUREJEA KWA SOKO LA WAZI KATIKA VIWANJA VYA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO-DSM

 Picha hizi za michoro zote zinaonyesha mpangilio jinsi gani Maumbo yatapangiliwa kwa ajili ya Wafanyabiashara wa Soko la Wazi katika Viwanja vya Shirika la Masoko ya Kariakoo.Katika siku chache zijazo Wafanyabiashara hao watarejea  na kuanza kufanya shughuli zao za kibiashara.

Katika michoro hiyo inaonyesha vizuri maumbo zaidi ya miambili yatakavyopangwa na kuacha njia katikati kwa ajili ya kupita Wateja/Wanunuzi wa bidhaa. Eneo hili lipo kati ya Jengo Kuu la Soko na Soko Dogo.