Tuesday, February 17, 2015

Bidhaa na Wafanyabiashara Sokoni Kariakoo-Jijini Dar Es Salaam.

 Limau ni moja ya viungo vnavyotumiwa sana na wapishi mbalmbali,Sokoni Kariakoo kuna kila aina ya bidhaa muhim unazozihitaji. Limau hizi huuzwa kwa bei ya rejareja na jumla. Eneo la shimoni ndiko hasa bidhaa hizi zinapatikana kwa wingi sana.

 Ndimu nazo hazijapungua hapa Sokoni Kariakoo,zinapatikana kwa wingi katika bei tofautitofauti kwa jumla na rejareja.Ndimu daraja la kwanza kabisa, fika Sokoni Kariakoo eneo la Shimoni.

 Mfanyabiashara huyu anayejulikana kwa jina la Munguatosha pichani hapo juu, yupo eneo la Shimoni yeye ni maalum tuu kwa uuzaji wa Karoti na pilipili hoho.Pia hupokea mazao kutoka kwa Wakulima mbalimbali kutoka mkoani,kama vile kutoka Wilayani Korogwe na Lushoto mkoani Tanga.
Bwana Dominik Zakayo ni miongoni mwa wafanyabiashara wa vitunguu saum na tangawizi katika Soko Kuu la Kariakoo eneo la Shimoni.Karibu ujipatie bidhaa mbalimbali.