Thursday, March 12, 2015

Ushirikishwaji wa Wadau katika maendeleo ni muhimu


Katika picha hizo hapo juu ni Wajumbe wa Kamati Kuu ya Uongozi wa Wafanyabiashara katika Soko Kuu la Kariakoo lililopo Jijini Dar Es Salaam,wakiwa katika Mkutano wa pamoja na Uongozi wa Shirika la Masoko Kariakoo. Mkutano huo ulikuwa na agenda kuu moja tuu ya kuwashirikisha Wafanyabiashara hao katika wazo la kuboresha matumizi ya sehemu ya maduka ya nyama(Mabucha) iliyomo ndani ya jengo la Soko Kuu la Kariakoo, kwa nia ya kuliongezea tija shirika. Kwenye picha ya chini aliyevaa miwani ni Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Florens Seiya akifafanua jambo kwa Wajumbe waliohudhuria mkutano huo juzi, mkutano huu ulifanyika ndani Ukumbi wa Mikutano wa Shirika.