Tuesday, June 17, 2014

Mkutano wa Mwaka wa 2SEEDS Network uliofanyika Korogwe Mkoani Tanga

 Katika picha hapo juu  ya kwanza juu  kushoto ni picha ya pamoja ya Wajumbe  wa Masoko Project kutoka Shirka la Masoko ya Kariakoo Jijini Dsm wajumbe hao kutoka kushoto ni Henry Rweijuna,Sophy,Anderson ShakaChristian Mlay,Monique na Munguatosha;picha ya pili juu ni Bwana Anderson Shaka akigawa kadi zenye namba kwa ajili ya kufanyia mazoezi ya kuuliza bei kwa njia ya SMS,picha ya chini kushoto ni Wajumbe wa Mkutano wakiwa katika chumba cha mkutano na picha ya chini kulia ni Mjumbe kutoka Masoko Project Bwana Christian Mlayi akitoa maelezo ya namna ya kutuma SMS ili kuuliza bei za mazao kutoka katika Soko Kuu la Kariakoo.
Katika picha hapo juu ni hekaheka za safari ya Wajumbe wa Masoko Project kutoka Dar Es Salaam. Hapa walikuwa wakisafiri kuelekea kijiji cha Tabora kilichopo nje kidogo ya mji wa Korogwe takribani KM 8 hivi;wakitumia usafiri wa bajaji hapo walikuwa wamenasa kwenye matope hivyo ikawalazimu kutelemka nakuanza kusukuma bajaji.
katika msafara huo alikuwepo Sophy,Munguatosha,Christian Mlay,Monique Galvalo,Henry Rweujuna,Anderson Shaka na madereva wa bajaji.
Vijiji vyenye miradi ya 2SEEDS Network Tabora,Kwakiliga,Kijungumoto,Bombomajimoto,Lutindi,Magoma vyote vipo katika Wilaya ya Korogwe.