Monday, June 2, 2014

Kariakoo Soko Kuu

 Katika picha hapo juu ni Mratibu wa Masoko Project Bi.Monique Galvao na wengine ni Wataalam wa kutengeneza Mifumo ya Kielekroniki kutoka Habari Mazao Team kijana Bariki na mwenzake Kaboda. Hapa walikuwa katika kikao kujadili namna ya kumalizia Project ya Masoko amabapo wao wanahusika katika uundaji wa mfumo saidizi ambao utafanya kazi sambamba na Mfumo mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo(KMC Database System) katika utoaji wa taarifa mbalimbali za bei za mazo yanayouzwa katika Soko Kuu la Kariakoo.Kikao hiki kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Shirika la Masoko mwishoni mwa wiki iliyopita.
Kutoka kushoto ni Bariki na Kaboda kutoka Habari Mazao Team wakiwa na Bwana Anderson Shaka yeye ni Mkuu wa Kitengo wa ICT katika Shirika la Masoko ya Kariakoo.Wote wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa kikao  kilicholenga kujadili na kuona jinsi Project ya Masoko itakavyomalizika na kuanza kuwanufaisha Wakulima,Wafanyabiashara pamoja na Walaji wa bidhaa zinazouzwa katika Soko Kuu la Kariakoo.