Monday, February 23, 2015

Aina mbalimbali za Mazao/Vyakula katika Soko Kuu

 Maboga nayo pia hupatikana hapa katika Soko Kuu la Kariakoo katika bei tofautitofauti,maboga ni miongoni mwa vyakula ambavyo hupendwa na watu wa kada tofauti.

 Viazi mviringo kutoka mikoa ya Nyanda za juu Kusini kama vile Njombe,Mbeya na Iringa, huingia Sokoni Kariakoo kila siku.
Vitunguu safiii kabisa kutoka mikoani Singida,Mbeya,Iringa na kwingineko huingia katika Soko Kuu la Kariakoo.