Wednesday, April 30, 2014

Sokoni Kariakoo leo!

 Mfanyabiashara Bwana Hussein akiwa ameegemea gari ambalo limebeba  Matikiti yake ambayo aliyafikisha Sokoni Kariakoo . Hapo alikutwa akiwa eneo la Soko la Jumla eneo maarufu kwa jina la Shimoni.
Eneo hilo katika picha hapo ni eneo la wazi lililopo kati ya Jengo la Soko Kuu la Kariakoo na Soko Dogo ambayo yote kwa pamoja yanasimamiwa na Uongozi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo. Kwa watu waliozoea siku zilizotangulia eneo hili lilikuwa ni eneo ambalo kila aina ya bidhaa za Matunda,Mbogamboga,Viazi na bidhaa nyinginezo zilikuwa zikiuzwa na Wajasiriamali/ Wafanyabiashara katika eneo hili; Lakini sasa kwa takribani mwezi sasa unakamilika pamekuwa wazi kama panavyoonekana kufuatia bomoa bomoa ya Manispaa ya Ilala kuingia hadi katika eneo hili la Soko.