Tuesday, September 2, 2014

Nyanya Bora zinapatikana Soko Kuu la Kariakoo

 Katika picha hapo juu ni Mama Mjasiriamali ambaye alijitambulisha kwa jina la Mama Shakila; Mama huyu hufanya biashara ya nyanya katika Soko Kuu la Kariakoo eneo la Shimoni kuanzia mapema asubuhi hadi jioni.Katika mahojiano aliniambia nyanya hizi kwa majira haya zinatoka mkoani Morogoro.
Sokoni Kariakoo ni mahali pekee amabapo unaweza kupata bidhaa bora na ambazo zinaweza kukidhi mahitaji yako ya kila siku kwa bei ya wastani.Kama katika picha hapo juu nyanya nzuri amabazo zipo katika kiwango safi cha ubora zinapatikana hapa sokoni. Ukifika Kariakoo tunakukaribisha katika eneo la Soko la jumula na rejareja eneo la Shimoni. Nyanya ni moja bidhaa kadhaa ambazo husafirishwa kwenda katika visiwa vya Commoro. Karibuni mjipatie bidhaa hizi bora!