Sunday, June 28, 2015

Soko Kuu Kariakoo Na Wakulima Vijijini

 Soko Kuu la Kariakoo haliishii tuu kupokea mazao yanayofika Sokoni badala yake sasa limekuwa likifanya ziara maalumu kuwatembelea wakulima walioko vijijini hasa katika Wilaya ya Korogwe kwa kuanzia, huku wakishirikiana na 2SEEDS Network shirika lisilokuwa la Kiserikali kutoka nchini Marekani kwa pamoja taasisi hizi mbili zimekuwa zikiwasaidia wakulima katika kuibua na kuendesha miradi mbalimbali ya kiuzalishaji mali, pia Soko  la Kariakoo likiwapa msaada zaidi kwakuwapa kipaumbele katika kupata soko la mazao wanayozalisha. Katika picha hapo juu ni moja ya mashamba ya wakulima hao walioko Korogwe Vijijini.

 Katika picha hapo juu ni Wanamtandao wa 2SEEDS Network wakiwa shambani wakiangalia maandalizi ya shamba yakiendelea. Mratibu wa mradi huo Bwana Cameron mwenye begi mgongoni alifika kijijini Bungu

Katika picha hapo juu ni shamba la mboga aina ya kabichi, shamba hili lipo katika kijiji cha Lutindi juu milimani kabisa Korogwe Vijijini. Mazao haya kwa kiasi kikubwa husafirishwa kuja  kuuzwa katika Soko kuu la Kariakoo Jijini Dar Es Salaam. Kwa ushirikiano wa 2SEEDS Network wakulima hawa wamekuwa wakizalisha kwa bidii mazao mbalimbali kama vile pilipili hoho,karoti,vitunguu maji, conflowers,bitroots n.k