Sunday, October 2, 2016

MENEJA MKUU MPYA AKABIDHIWA OFISI -SHIRIKA LA MSOKO KARIAKOO SEPT.30,2016

 Picha hiiya pamoja ambayo inaonyesha tukio la kumkaribisha Meneja Mkuu mpya wa Shirika la Masoko Kariakoo siku ya Ijumaa tarehe 30.9.2016 mchana. Hafla hii fupi ilifanyika katika Ofisi za Shirika hili zilizopo katika Jengo Kuu la Soko Kuu la Kariakoo.Aliyeketi katika kiti ni Meneja Mkuu mpya wa Shirika Bwana Hetson Kipsi, na waliosimama kutoka kushoto ni Bwana Mlelo Mgheni Meneja Biashara na Mipango wa Shirika, Bwana Denisi Mfuruki ni Mjumbe wa Bodi ya Shirika,Bwana Cprian Kuyava kutoka Hazina ambaye pia  ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi, Bwana Dk. Buhohela Lunogelo ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika, Bwana Florens Seiya aliyekuwa Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko na sasa amemaliza muda wake wa Utumishi katika Shirika hili. Anayefuata ni Meneja Utumishi na Utawala wa Shirika Bwana Godwin Mroso, Bwana Mathias Mbafu Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi katika Shirika,Meneja wa Fedha Bi.Marieta Masaua ambaye ni Meneja wa Fedha katika Shirika,Bwana Donald Sokoni Meneja wa Afya na Usafi,Bwana Josam Mnzava Mkuu wa Kitengo cha Usalama,Bwana Paul Kiwera Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi cha Ndani,na Bwana Flavian Mlelwa Kaim Mkuu wa Kitengo cha Matunzo.
 Wakati wa makabidhiano ya Ofisi  Dua na Sala fupi zilifanyika ndani ya Ofisi ya Meneja Mkuu kama ishara ya kumuombea mafanikio Meneja Mkuu aliyekuwa akimaliza muda wake na kadhalika kama ishara yakumuombea Meneja Mkuu mpya wa Shirika kupata ufanisi kiutumishi na hekima ya Mungu imuongoze katika utekelezaji wa majukumu yake kama Mtumishi wa Umma mwenye kuwatumikia Watanzania.



 Meneja Mkuu mpya Bwana hetson Kipsi akizungumza na Menejimenti ya Shirika  pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Masoko Kariakoo katika kikao kifupi cha kukabidhiwa Ofisi. Meneja Mkuu huyo mpya alisisitiza ufanisi na uwazi pamoja na kujituma katika Utumishi ndani ya Menejimenti. Mambo hayo ya msingi ndiyo hasa yatakayo lisaidia Shirika hilo kupiga hatua ya kimaendeleo. Lakini alionya tabia ya uzembe kwa Watendaji wa Shirika jambo ambalo alisema hatalivumilia hata kidogo katika uongozi wake katika Shirika hili kongwe lililoanzishwa Mwaka 1974 kwa mujibu wa Sheria ya Bunge Namba36, ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Meneja Mkuu  Bwana Florens Seiya aliyemaliza muda wakeakitoa hotuba fupi ya kuelezea mwenendo mzima wa Shirika mbele  ya Meneja Mkuu mpya Bwana Hetson Kipsi na Mwenyekiti wa Bodi pamoja na Wajumbe wa Menejimenti ya Shirika hilo muda mfupi kabla ya makabidhiano ya ya Ofisi, Ijumaa tarehe 30.9.2016 mchana. Hafla ilyofanyika katika Ofisi za Soko kuu la Kariakoo Jijini Dar Es Salaam.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika Bwana Dk.Buhohela Lunogelo akipeana na  mkono wa na Meneja Mkuu aliyemaliza muda wake wa Utumishi katika Taasisi hii. Anayetazama kwa karibu hapo ni Bwana Hetson Kipsi Meneja Mkuu mpya wa Shirika. Mwenyekiti wa Bodi huyo alimshukuru Meneja Mkuu aliyemaliza muda wake wa Utumishi na kumtakia heri katika muda wake wa utumishi uliobakia katika kuutumikia Umma. Kadhalika alimkaribisha Meneja Mkuu Mpya Ofisini.Bwana Kipsi alikuwa Mtumishi katika Wizara ya TAMISEMI ambayo ipo chini ya Ofisi ya Rais.Meneja huyu mpya ni Mtaalam wa Uchumi kwa taaluma yake.
 Katika picha hapo juu ni moja ya Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Denis Mfuruki mwenye karatasi mkononi akipeana mkono na Meneja Mkuu mpya wa Shirika  hilo Bwana Hetson Kipsi kama ishara ya upendo kumkaribisha Mtendaji Mkuu huyo mpya katika Ofisi ya Meneja Mkuu. Aliyesimama kushoto ni Bwana Florens Seiya ambaye amemaliza muda wake wa kuhudumu katika Shirika hili, baada yakufanya kazi hapa katika kipindi cha miaka saba.Mabadiliko haya ya Uongozi yamekuja baada ya Uteuzi mpya alioufanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dk.John Magufuli mapema mwanzoni mwa mwezi Septemba mwaka huu.
Hapa katika picha ni Meneja Mkuu Bwana Florens Seiya akipeana mkono na Meneja Mkuu mpya wa Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Hetson Kipsi. Mameneja hawa walipeana mikono Ofisini katika Ofisi ya Meneja Mkuu wakishuhudiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Masoko, Makamu Mwenyekiti wa Bodi pamoja na Menejimenti ya Shirika hili,siku ya Ijumaa tarehe 30.9.2016 mchana.