Monday, August 24, 2015

Matukio katika Picha

 Katika picha hapo juu kutoka kulia ni Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko Kariakoo Bwana Florens Seiya, Mwenyekiti wa TUICO tawi Bwana Dennis Mfuruki aliyesimama na Bwana Henry Rwejuna ambaye ni Katibu wa TUICO tawi, kwa pamoja wakiwa wanaendesha mkutano wa wafanyakazi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo mwishoni mwa wiki iliyopita. Ni moja ya mikutano ya kawaida ambayo imekuwa inafanyika kwa nia ya kujenga na kuimarisha mahusiano baina wafanyakazi wa shirika na Mwajiri wao, wakilenga zaidi hali ya mwenendo mzima wa Shirika.
 katika picha hapo juu ni vitunguu maji ambavyo ni moja ya bidhaa zinazouzwa hapa katika soko  Kuu la Kariakoo jijini Dar Es Salaam.Vitunguu maji hivi hufikishwa sokoni Kariakoo vikiwa vinatoka mikoa mbalimbali ya Tanzania kama vile Mbeya,Arusha,Iringa na Singida.
Picha hiyo hapo juu inaonyesha sehemu tuu ya Watumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo wakiwa wametulia huku wakifuatilia maelezo ya Meneja Mkuu wa Shirika ,pichani hapo juu hayupo wakati wa mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Shirika mwishoni mwa wiki iliyopita.

Thursday, August 20, 2015

SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO



TANGAZO LA KAZI

Shirika la Masoko ya Karikaoo ni Shirika la Umma lililoanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Bunge Na.32 ya mwaka 1974 na kupewa majukumu ya kusimamia na kuendesha Soko Kuu la Kariakoo pamoja na Masoko mengine yatakayokuwa chini ya usimamizi wa Shirika pia kujenga Masoko mengine mapya katika Jiji la Dar es Salaam na kusimamia uendeshaji wake. Shirika linakaribisha maombi ya nafasi  mbili za kazi zifuatazo:
  1. Mwanasheria  Daraja la 11
Muombaji awe na Shahada ya Sheria kutoka Chuo Kikuu kinachotambuliwa na Serikali. Awe amepitia Shule ya Sheria na kusajiliwa kama Wakili.
Kazi na Majukumu.
Kushauri masuala ya kisheria katika Shirika la Masoko ya Kariakoo.
Kuandaa nyaraka zote za kisheria kwa ajili ya kusaidia kufikia malengo ya Shirika.
Kufuatilia na kutunza kumbukumbu muhimu kwa ajili ya kutumika kwenye mashauri Mahakamani.
Kuandaa mihutasari ya mashauri mbalimbali ya shirika yaliyopo mahakamani.
Kuandaa na kupeleka notisi za kisheria kwa wadaiwa wa shirika  .
Kufanya shughuli yeyote atakayo pangiwa na Meneja Mkuu au Mkuu wa kitengo.
  1. Ofisa Ugavi Msaidizi
Muombaji awe na Stashahada ya katika fani ya ununuzi na ugavi, awe amesajiliwa na PSPTB
Kazi na Majukumu.
Kuhakikisha kuwa vifaa vinavyonunuliwa vinapokelewa na kuingizwa katika vitabu vya Shirika..
Kuhakikisha kuwa nyaraka zote za stoo zinajazwa kwa ufasaha na kwa wakati.
Kuhakikisha kuwa mali zote zilizoifadhiwa stoo zinatuzwa  bila upotevu wowote.
Kuhakikisha kuwa uingizaji na utoaji wa bidhaa unafuata sheria na kanuni za manunuzi ya umma.
Kuhakikisha kuwa vifaa na mali zinazohifadhiwa stoo zinatunzwa katika mpangilio mzuri
Kufanya kazi zozote atakazopangiwa na Mkuu wa Kitengo.
MASHARTI YA JUMLA
Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45
 Waombaji wote waambatishe nakala ya cheti cha kuzaliwa. Na picha (passport size) moja ya rangi
Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
Maombi yote yaambatane na nakala za vyeti vya kidato cha nne na kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na nakala ya  vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.

Mwisho wa Kupokea maombi ni 29/08/2015.

Maombi hayo yatumwe kwa :

Meneja Mkuu,
Shirika la Masoko ya Kariakoo,
P.O.BOX 15789,
Dar es Salaam.
Na kwa Email: info@kariaakoo.or.tz.


Thursday, August 13, 2015

TANGAZO MAALUM



SHIRIKA LA MASOKO KARIAKOO
(KARIAKOO MARKETS CORPORATION)



AP/109/KMC/2015/2016/C

Expression of Interest



For

PROVISION OF CONSULTANCY SERVICES

Date: 10th August 2015
1.   The Kariakoo Markets Corporation has set aside funds towards the cost of providing consultancy services as described below and it intends to apply part of the proceeds of this fund to cover eligible payments under the contract.

S/N
TENDER DESCRIPTION
LOT/TENDER NUMBER
01
Preparation of Strategic plan (2015 – 2018)
PA/109/2015/2016/STP/C/01
02
Valuation of Assets
PA/109/2015/2016/VA/C/01

2.   The Kariakoo Markets Corporation now invites eligible registered Local Consultancy firms to indicate their interests in providing the services mentioned above.

3.   Interested individual consultants must provide information indicating that they are qualified to perform the services by submitting consultant’s profile, description of similar assignments, experience in similar conditions, availability of appropriate skills among staff, etc.

4.   A consultant will be selected in accordance with the procedures set out in the Public Procurement Act 2011 and the Public Procurement Regulations – Government Notice No. 466 of 2013.

5.   Interested eligible consultants may obtain further information from the office of the Tender Board Secretary, Kariakoo Markets Corporation, P.o.Box 15789, Dar es Salaam from 08:30am to 03:30 pm on Monday to Friday inclusive except on public holidays.

6.   Expressions of Interest (EoI) must be delivered to the address below not more than 25thAugust 2015 at or before 10:00hrs.

The Secretary,
Kariakoo Markets Corporation Tender Board,
P.o.Box 15789,
Dar es Salaam.

7.   Closing date for receiving the expression of interest is 25thAugust 2015 at 10:00. Late Expressions of Interest shall not be accepted for evaluation irrespective of the circumstances.



General Manager
Kariakoo Market Corporation

WANAMTANDAO WA LUTINDI-KOROGWE

Miongoni mwa miradi ambayo imepata mafanikio makubwa inayosimamiwa na 2SEEDS Network wilayani Korogwe Vijijini ni ule uliopo katika kijiji cha Lutindi. Mradi huu unastawisha mazao ya mbogamboga kama vile inavyoonekana katika picha hapo juu shamba la moga aina ya kabichi linavyoendelea kutunzwa na wanakikundi.Mbali na mboga aina ya kabichi pia wanazalisha pilipili hoho,bitroots,bilinganya na nyanya chungu.