Wednesday, July 16, 2014

Bodi ya Ushauri ya Shirika la Masoko ya Kariakoo.

 Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Wilson Kabwe ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Jiji la Dar Es Salaam akiendesha Mkutano wa Bodi hiyo jana Jumanne tarehe 15/7/2014.Mkutano huo maalum ulifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Shirika la Masoko ya Kariakoo.Mkutano huo ulipokea taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha wa 2013/2014; na hatimaye Bodi hiyo  ilipokea Bajeti mpya ya Shirika kwa mwaka  wa fedha 2014/2015 kuijadili na kuipitisha.
 Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo Bwana Florens Seiya akiwakaribisha Wajumbe wa Bodi ya Ushauri katika Mkutanoo huo maalum wa kupokea taarifa ya utekelezaji wa Bajeti ya mwaka wa fedha wa 2013/2014 na hatimaye kupokea na kuijadili na kuipitisha bajeti ya mwaka wa fedha  wa 2014/2015.Aliye upande wa kushoto mwenye shati  nyeupe ni Kaimu Meneja wa Biashara na Mipango wa Shirika bwana Mrero Mgheni.
 Baadhi ya Wajumbe wa Bodi wakiwa Ukumbini bado wameketi Ukumbini mara baada ya Mkutano kumalizika.
Baadhi ya sehemu ya Wajumbe waliohudhuria  Mkutano wa Bodi ya Ushauri ya Shirika la Masoko ya Kariakoo jana Jumanne 15/7/2014.