Tuesday, May 27, 2014

Sample za Maumbo yatakayotumika katika Soko la Wazi

 Katika picha ni "sample" ya maumbo ambayo yanatarajiwa kutumika Sokoni Kariakoo katika Soko la Wazi ambapo kwa sasa hapajaanza kutumiwa na Wafanyabiashara tangu Manispaa ya Ilala walipovamia na kubomoabomoa meza zilizokuwa zinatumiwa na Wafanyabiashara hao mapema mwanzoni mwa mwezi wa Aprili 2014.Waliosimama na kuziangalia ni Afisa Biashara  Bwana Vedastus Valentine mwenye shati la bluu na Mhandisi wa Shirika Bwana Flavian Mlelwa.
Wafanyabiashara watakuwa wanapanga bidhaa zao humu katika Maumbo haya na kuwauzia Wateja, Maumbo haya yanakusudiwa kuanza kutumika katika eneo la Soko la Wazi katika Viwanja vya Shirika la Masoko ya Kariakoo katika siku chache zijazo mara baada ya taratibu zote kukamilika.

No comments:

Post a Comment