Wednesday, June 10, 2015

Wanamtandao

Katika picha hapo juu ni ya Wanamtandao amabao wameunganishwa na Shirika la 2SEEDS Network ambao wamo katika vikundi tofautitofauti kutoka katika miradi mbalimbali ipatayo nane na ambayo imesambaa katika vijiji mbalimbali vilivyomo katika wilaya ya Korogwe Vijijini. Vijiji hivyo ni hivi vifuatavyo Kwakiliga,Tabora,Magoma, Magoma Kwata, Bombo Majimoto,Kijungumoto,Lutindi na Bungu.

Katika vijiji hivyo kuna miradi mbalimbali ya uzalishaji mali kama vile ufugaji nyuki,kuku na mbuzi na kilimo cha mazao mbalimbali.

Tutakuwa tunawaletea taarifa za mradi mmojammoja kila siku hadi mwisho.

No comments:

Post a Comment