Tuesday, April 1, 2014

USAFI NI SEHEMU YA MAISHA YETU SOKO KUU LA KARIAKOO

Shirika la Masoko ya Kariakoo (SMK), huzingatia sana suala zima la Usafi katika maeneo yake kila siku. Katika picha hapo juu ni Gari mojawapo kati ya mengi likiwa eneo la Shimoni likiwa linapakia takataka; hufanya kazi ya kuondoa takataka zinazozalishwa Katika Soko Kuu la Kariakoo kutokana na uingizwaji wa bidhaa mbalimbali toka mikoani.Magari haya hufanya kazi Usiku na Mchana ili kuhakikisha eneo la Soko  Kuu la Kariakoo linakuwa safi muda wote.
Katika picha hapo juu ni Bwana Seifu Abdalah ambaye  ni Mtumishi wa Shirika la Masoko kutoka katika Idara ya Usafi,alikutwa eneo la Shimoni akikagua mifereji ya Majitaka inayopita eneo hilo ili kuhakikisha Mfumo mzima wa maji taka upo sawa sawa.Kutokana na umuhimu wa Mfumo huu wa majitaka katika miundombinu ya Soko hili ukaguzi kama  huu hufanyika kila siku na mara kwa mara.

No comments:

Post a Comment