Thursday, April 10, 2014

Matumaini mapya kwa Wafanyabiashara Sokoni Kariakoo!

 Katika picha hapo juu ni jopo la Wakaguzi wa ndani wa Shirika la Masoko ya Kariakoo wakiangalia ubora wa maumbo amabayo yaliletwa katika Ofisi za Shirika  jana.Maumbo hayo yakiisha kuthibitishwa yataanza kutumika katika eneo la Soko la Wazi lililopo kati ya Jengo Kuu la Soko na Soko Dogo ambapo Wafanyabiashara  watayatumia kupanga bidhaa zao mablimbali humo na kuwauzia wateja.Wakaguzi hao wakiongozwa na Mkuu wao Bwana Paul Kiwera aliyevaa kitambulisho kutoka kulia, Bwana Ncheya Kulwa na Bwana Longino .A.k.a Mkulu wa Bangoye!
Katika picha hapo juu ni "Sampo"(sample) ya maumbo ambayo yanatarajiwa kutumiwa na Wafanyabiashara ambao mapema wiki  iliyopita walibomolewa meza zao katika eneo la Soko la  Wazi la Kariakoo.Eneo hilo ni sehemu ya Kiwanja cha Soko Kuu la Kariakoo. Wafanyabiashara hao watakuwa wanatumia maumbo hayo kupanga bidhaa zao mabalimbali wanazoziuza sokoni hapo.

No comments:

Post a Comment